Monday, November 3, 2014

Cellulite unayo ama hauna? Jinsi ya kuondoa Cellulite

 
Cellulite ama kwa jina lingine cottage cheese ni sehemu ya ngozi nene ambayo hutokea kutokana na mafuta yanayojaa chini ya ngozi na hivyo kusababisha kukata mzunguko wa damu (blood circulation) katika sehumu hizo. Kwa kawaida wanawake wengi ndo huwa na cellulite ila hata wanaume pia. Cellulite huonekana zaidi katika sehemu za mapaja, nyama za mikono, maeneo ya tumboni na hata miguuni. 
Cellulite husababisha mabonde bonde kwenye ngozi kutokana na mafuta yaliyojaa chini ya ngozi.
Ultrasonic massage treatment– Hii massage treatment ni ya moto inayofanywa na kimashine kinachopitishwa juu ya ngozi (mahali penye cellulite). Treatment hii husadia kuchoma na kusaidia stimulation na circulation of blood around the cottage cheese area (unahitaji about 10 treatment) ila hata ukishafanya hizi treatment inabidi uendelee kuzifanya  kila baada ya muda flani bila hivyo cellulite inarudia pale pale.
  
 

Mafuta yaliyojaa chini ya ngozi yanayosababisha mabonde mabonde kwenye ngozi






Ila Dr. Oz wa Dr. Oz Show anashauri kufanya mazoezi na kuwa na diet safi (kuacha kula vitu vyenye mafuta sana badala yake kula matunda zaidi na kunywa maji kwa wingi). Anasema kwamba massages na liposuction haisaaidii, kwasababu sana sana, kitu massage inachofanya ni kusugua ile sehemu yenye mafuta (cellulite) na kuyarudisha chini kwa muda halafu baada ya wiki ngozi inajirudia na kustreach na mimafuta (cellulite) inarudia pale pale. Liposuction pia ndo hivyo hivyo, ni procedure inayo fyonza mafuta kupitia machine lakini watu wanachosahau ni kwamba mafuta haya yanapofyonzwa lile eneo lilobaki linatepeta/tupu (chukulia mfano wa tobo lililojazwa mafuta ukiyatoa mafuta sio kwamba tobo ndo litajiziba, litabaki pale pale na mafuta mengine yatakuja tena kujirundika). Hivyo ndo maana hata ukiamua kwenda chini ya kisu ama machine kuyafyonza ama kukata haya mafuta sana sana ni kujiongezea tuu kazi na gharama in the long run. 
Hivyo basi, madocta hawa wanashauri kwamba kitu kikuu ni kufanya mazoezi haswa kama kukimbia na kutembea haraka haraka., pia elipticals, na muscle toning. Hizi ndo njia pekee zilizoonyesha kusaidia kuondoa cellulite kabisa.  
 




Ama unaweza kutumia njia za kienyeji kama kawaida…(home remedy)
Mahitaji:
1 – Chumvi kijiko cha chakula
1 – Kikombe cha water
½ – Juice ya limao
½ – (pilipili nyekundu iliyosagwa) cayenne pepper
Changanya maji na chumvi. Then ongeza juice ya limao, then ongezea cayenne pepper.
Koroga mchanganyiko wako. Halafu paka kwenye maeneo uliyo na cellulite. Acha mchanganyiko wako ukae kwa muda kwenye ngozi halafu osha ama oga na maji safi. Endelea kufanya hivi kwa muda na kuendelea mpaka uone matokeo mazuri ama uridhike mwenyewe. 


0 comments:

Post a Comment